KAKOBE AKANA KUKWEPA KODI,ASEMA TAARIFA ZA TRA ZA KISHILAWADU
Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Followship (FGBF), Zachary Kakobe amekanusha taarifa za Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwamba kanisa lake linakwepa kodi.
Akizungumza leo Jumapili Februari 25, 2015 katika kanisa hilo lililopo Mwenge, jijini Dar es Salaam Kakobe amewataka waumini wa kanisa hilo kuzikataa taarifa hizo na kwamba zimejaa siasa,ni za kishilawadu
SOMA ZAIDI-TRA yaingia matatani kwa taarifa ya kanisa la Askofu Kakobe, yatoa ufafanuzi
Kakobe ametoa ufafanuzi huo zikiwa zimepita siku nne tangu TRA kutoa taarifa ya uchunguzi katika kanisa hilo na kubaini mambo saba.
SOMA ZAIDI-VIDEO-TRA yabaini mambo saba ukaguzi kanisani kwa Askofu Kakobe

No comments: